TUHUMA ZA KUWAPATIA UJAUZITO WANAFUNZI SENGEREMA ZAWASIMAMISHA KAZI WALIMU WAWILI.



Na, Paulina Mpiwa, Sengerema- Mwanza

Mkuu wa Wilaya ya sengerema mkoani Mwanza   Bwn, Emmanuel Kipole amemwagiza mkurugenzi mtendaji wa halimashauri ya Buchosa Wilayani Sengerema  kuwasimamisha kazi walimu  wawili wanaotuhumiwa kuwapatia ujauzito wanafunzi.

Amewataja walimu hao kuwa ni mwalimu Robert Malewa Albano wa shule ya Sekondari Iligamba   anayetuhumiwa kumpatia ujauzito mwanafunzi wa kidato cha kwanza   na kukatisha masomo yake huku ,    na mwalimu wa shule ya Msingi Kasisa Oscar Mkandya akituhumiwa kumpatia ujauzito mwanafunzi wa kidato cha tatu kisha kumshawishi kutoa ujauzito huo.

Kauli hiyo ameitoa   katika  Kata  ya Nyehunge Halimashauri ya Buchosa  wakati  akizungumza na  watendaji wa halimashauri pamoja na madiwani wa halimashauri hiyo kuhusu suala la kusimamia elimu katika maeneo yao.

Kipole amesema kazi ya walimu ni kuwalea wanafunzi katika maadili mema kuwafundisha ili wapate elimu bora na hakuna mtaala unaelekeza mwalimu kumpatia ujauzito mwanafunzi.


Amesema viongozi wote wanapaswa kusimamia sheria kanuni na  maadili ya utumishi wa Umma kwa kufanya kazi kwa weledi mkubwa.



Upande wake Mkurugenzi wa Halimashauri ya Buchosa Bw. Crispin Luanda,  ameahidi kutekeleza agizo hilo   lililotolewa na mkuu wa wilaya  ili kudumisha nidhamu  kwa watumishi   wote wa  umma.

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 Response to "TUHUMA ZA KUWAPATIA UJAUZITO WANAFUNZI SENGEREMA ZAWASIMAMISHA KAZI WALIMU WAWILI. "

Post a Comment