UCHAFU WA MAZINGIRA KAHAMA WATUMBUA VIGOGO WAWILI WA IDARA YA USAFI



 
Na Salvatory Ntandu 
KAHAMA
Halmashauri ya Mji wa Kahama leo imewasimamisha kazi Wakuu wa idara ya Usafi na Mazingira kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kusimamia usafi na mazingira ya mji huo.
Akizungumza na Kahamafm Mkurugenzi wa Halmashauri ya hiyo ANDARSON MSUMBA amesema waliosimamishwa kazi ni pamoja na Mkuu wa idara ya usafi na mazingira MARTINE MASELE, Afisa afya DEOGRATIUS DOTTO, na afisa mazingira JOHANNES MWEBESA.
MSUMBA amesema Watumishi hao wameshindwa kusimamia  usafi na mazingira na kupelekea mrudikano wa taka katika vizimba hali inayoweza kuhatarisha usalama wa afya za wananchi kutokana na vizimba hivyo kuwa karibu na makazi ya watu.
Amefafanua kuwa katika kizimba cha Milangokumi, na kwamamafarida kuna taka nyingi zilizosambaa ovyo ikilinganishwa na vizimba vya Nyahanga na Nyihogo na amewahakikishia wananchi usalama kwani taka hizo zitakuwa zinazolwa kila siku.
Mbali na hilo MSUMBA ametoa rai kwa wananchi kutunza mazingira katika maeneo yao ikiwa ni pamoja  kuwa na vipokea taka.
      
Uamuzi huo umefikiwa baada ya jana  Naibu Waziri wa nchi Ofisi ya Makamo wa Raisi Mazingira LUHAGA MPINA kufanya Ziara ya kukagua usafi wa mazungira  katika Halmashauri ya Mji hiyo.



TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 Response to "UCHAFU WA MAZINGIRA KAHAMA WATUMBUA VIGOGO WAWILI WA IDARA YA USAFI"

Post a Comment