ABIRIA WALIA KUCHELEWESHWA SAFARI ZAO MKOANI GEITA.



Na, Paulina Mpiwa, Geita.

Baadhi ya abiria  katika  kituo  cha   magari madogo   Mkoani Geita  wamewalalamikia   tabia  ya  baadhi  ya   madereva kuwakatia   tiketi  na   kushindwa kuondoka kwa  wakati,  jambo ambalo linasababisha kuchelewa safari zao.   

Wakizungumza  na  Mulika Jamii   abiria  hao    wamesema  pindi wanapofika katika  kituo hicho  madereva   wa vyombo  hivyo   huwaagiza   wapiga debe   kuwapokea abiria kwa  kuwavuta  kwa nguvu   kupanda  usafiri wao  na kuchelewa kuondoka, kitendo ambacho wamedai kuwa ni  unyanyasaji wa abiria.    

Madereva wa vyombo vya moto wamekiri kuwepo kwa hali hiyo na  kusema   kuwa  kwa sasa wamekaa kikao na kuweka utaratibu mzuri wa kuanza safari zao mapema ili kuondoa usumbufu  unaojitokeza  kwa  sasa.

Nae mwenyekiti  wa    chama cha madereva mkoa wa  Geita  Bwn, Faustine John  ,amesema   kuwa suala la wapiga debe kuwanyanyasa abiria halikubaliki  kwa kuwa kazi yao kubwa ni kuwaonyesha abiria usafiri pekee na si vinginevyo.

Kwa upande wake  Afisa Leseni  mkoa wa Geita Bwana, Haghai  Emil  amewataka  abiria pale wanapokumbana na changamoto ya kucheleweshwa  safari zao  watoe taarifa katika idara husika ili watu hao wachukuliwe hatua zaidi za kisheria.


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 Response to "ABIRIA WALIA KUCHELEWESHWA SAFARI ZAO MKOANI GEITA."

Post a Comment