HALMASHAURI YA BUCHOSA SENGEREMA YAIBUKA KIDEDEA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MWANZA.



Na Paulina Mpiwa, Sengerema Mwanza.

Halimashauri ya Buchosa Wilayani Sengerema Mkoa wa Mwanza imetajwa kuwa ya kwanza kati ya halmashauri saba za mkoa wa mwanza katika utoaji wa huduma  bora  za afya kwa wananchi katika maeneo yao.

Mkuu wa Wilaya ya Sengerema   Bwn, Emmanuel Kipole amesema hayo katika kata ya Nyehunge halimashauri ya Buchosa alipokuwa kizungumuza na watendaji wa halimashauri hiyo katika kuweka mikakati madhubuti ya kuzidi kuboresha huduma za afya.

Amesema kuwa Buchosa imetangazwa kuwa ya kwanza katika kuboresha vituo vya  afya na huduma nzuri kwa wananachi  katika kikao cha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongera pamoja na katibu tawala wa mkoa.  

Kwa upande wake   Mganga Mkuu wa Halimashauri hiyo Dr Ernest Chacha amesema kuwa usimamizi , na ufuatiliaji kutoka timu ya halimashauri ikiongozwa na mganga mkuu  pamoja na kushirikiana na watumishi wa afya katika halimashauri hiyo ndiyo umeifanya Buchosa kuibuka kidedea  katika mkoa wa mwanza.



Aidha baadhi ya wananchi wa eneo hilo wamepongeza hatua hiyo na kuiomba wizara ya afya kuendelea kuboresha zaidi huduma zake hasa  dawa ili kumrahisishia mwananchi wa kipato cha chini kupata huduma zote muhimu katika vituo vya kutolea tiba vya serikali.   

TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 Response to "HALMASHAURI YA BUCHOSA SENGEREMA YAIBUKA KIDEDEA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA MKOA WA MWANZA."

Post a Comment