fisi anayedaiwa kusababisha kifo cha Mwanamke kahama |
Na salvatory kelvin
KAHAMA
Mwanamke mmoja aliyetambuliwa
kwa jina moja la MARIDADI anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 35 Mkazi wa
Kijiji cha Nyang’wale katika Halmashauri ya Mji wa Kahama na ambaye alijeruhiwa
vibaya na fisi leo alfajiri akienda kuteka maji, amefariki dunia.
Akithibitisha kifo hicho,
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Kahama, DR. EMMANUEL KADELYA ameiambia
Kahama FM jioni hii kuwa MARIDADI amefariki dunia wakati akisafirishwa kwenda
Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza kwa matibabu zaidi.
Mapema leo mchana, Daktari
wa upasuaji katika chumba cha upasuaji cha hospitali hiyo, Dr. GEORGE MASASI alisema
MARIDADI alifikishwa katika hospitali hiyo majira ya saa 3 asubuhi akiwa
mahututi kutokana na majeraha makubwa aliyosababishiwa na fisi huyo.
Mwandishi wetu aliyetembelea
Hospitali ya Wilaya ya Kahama mapema leo asubuhi alishuhudia Mwanamke huyo
akiwa hajitambui akiwa amenyofolewa pua, taya la juu kulia, jicho la kulia
pamoja na baadhi ya nyama katika shavu la kulia huku ulimi wake ukining’inia
nje.
0 Response to "SHIDA YA MAJI NYANG'WALE YASABABISHA KIFO CHA MWANAMKE KWA KULIWA NA FISI"
Post a Comment