BEI NDOGO NA PEMBEJEO MBOVU ZAWALIZA WAKULIMA WA ZAO LA PAMBA SENGEREMA.




Na,Paulina Mpiwa , Sengerema Mwanza.

Imeelezwa     kuwa   bei ndogo   ya zao la pamba, pembejeo mbovu    na   mbolea kupanda  bei   ni chanzo  kikubwa  kilichosababisha     wakulima wengi  wa   zao la pamba  Wilayani  Sengerema  mkoani Mwanza   kuacha  kulima zao hilo.

Kauli hiyo imetolewa na baadhi ya wakulima wa zao la pamba Wilayani Sengerema ambapo wamedai    kuwa  licha  ya  kutumia gharama kubwa  kulitunza zao  hilo ,lakini huuza kwa bei ndogo hali inayowakatisha  tamaa kuendelea kulima.

Wakulima hao wameeleza kuwa kama  serikali itaongeza bei ya pamba  ,kuboresha pembejeo na kushusha bei ya mbolea wataendelea kulima zao hilo kwa kuwa ndio mkombozi kwa wakulima kama zao labiashara.

Hata hivyo wameiomba serikali kutazama kilimo cha pamba kwa jicho la tatu  ikiwemo kukifufua  kwa kutoa mahitaji muhimu ya zao  hilo   mapema   pindi msimu  wa kilimo cha  pamba   unapofika    ili  wakulima waondokana na umasikini.  

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Sengerema ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Pamba Wilaya Bwn,Emmanuel Enock Kipole amekiri kuwepo kwa  baadhi ya changamoto hizo na kusema kuwa serikali tayari imekwishaliona hilo na mpaka sasa baadhi ya changamoto zimeanza kufanyiwa kazi  ikiwemo wakulima kupatiwa  mbegu zenye ubora.

Aidha Bwn. Kipole amesema suala la bei serikali pia inaendelea kulishughulikia ili kuhakikisha mkulima wa zao la pamba ananufaika na kilimo hicho kwa kuuza kwa bei inayokubalika


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 Response to "BEI NDOGO NA PEMBEJEO MBOVU ZAWALIZA WAKULIMA WA ZAO LA PAMBA SENGEREMA."

Post a Comment