Na Salvatory Kelvin
Mkazi wa Kitongoji cha Buyange Kijiji cha Ikinda wilayani Kahama LUCAS
SAMSON(40), leo amehukumiwa kwenda jela miaka 20 kwa kosa la kumdhalilisha mtoto
wa kike wa miaka 8 kwa kumwagia mbegu za kiume sehemu zake za siri.
Hukumu hiyo imetolewa na
Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya hiyo, IMANI BATENZI baada ya kuridhika na
ushahidi uliotolewa na upande wa Mashitaka pamoja na Ripoti ya uchunguzi wa
Daktari.
BATENZI amesema Mahakama
imetoa adhabu hiyo licha ya SAMSON kushindwa kuongea na kwamba mahakama haiwezi
kusita kutoa adhabu kwa mtuhumiwa kwa sababu ushahidi uliotolewa unatosheleza
kumtia hatiani.
Awali Mwendesha Mashitaka wa
Polisi, SAADA ADAM amesema katika shauri hilo nambari 780/2016 kuwa SAMSON
alimdhalilisha mtoto huyo Desemba 16 mwaka jana katika kijiji hicho cha Ikunda
kwa kumwagia mbegu za kiume katika sehemu zake za siri.
Hakimu BATENZI amesema
SAMSON atatumikia kifungo cha miaka 20 gerezani ili iwe onyo na fundisho kwa
Wanaume wengine wenye tabia kama hiyo ya kuwadhalilisha watoto.
0 Response to "ALIYEJARIBU KUBAKA MTOTO WA MIAKA 8 AHUKUMIWA JELA MIAKA 20"
Post a Comment