DC SENGEREMA AFUTA BMU ZOTE MAPAMBANO DHIDI YA UVUVI HARAMU.



Na, Paulina Mpiwa, Sengerema Mwanza.



                                                  Mkuu wa wilaya ya Sengerema Bw. Emanuel Kipole

Mkuu  wa  Wilaya   ya  Sengerema    Mkoani Mwanza  Bwn, Emmanuel    Enock    Kipole     amefuta    kamati   ndogo    zote   za  utunzaji wa  Mazingira  na rasilimali za fukwe ziwa Victoria  (BMU)   Wilayani Sengerema     kutokana   na    kuendelea    kushika kasi kwa uvuvi haramu.         

Mkuu wa wilaya    ametoa maamuzi hayo     katika baraza la madiwani  lililofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ambapo amesema  kuwa licha ya kuwepo kamati hizo lakini bado uvuvi haramu   unaendelea kushamili katika ziwa hilo. 


Pia ,Bwn,Kipole ametoa siku  tatu kwa    diwani wa kata ya chifumfu  Robart Madaha kurejesha  makokoro yote ya  wavuvi haramu  yaliyopo  katika kata yake  na kuyapeleka  mwenyewe katika    kituo cha polisi cha Wilaya ya Sengerema na  kama   hatafanya hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.  


Baada ya kutoa maagizo hayo  kwa  diwani huyo   Mkuu wa wilaya  pia   ameliagiza jeshi la polisi  Wilaya ya Sengerema     kuwakamatwa   mara moja  Afisa mtendaji  wa kata  na mwenyekiti wa kijiji cha Nyakaliro  kwa kile alichodai  ni kukumbatia suala la uvuvi haramu katika maeneo yao. 


Katika hatua nyingine mkuu huyo wa wilaya amekemea kitendo cha  baadhi ya viongozi wanaosaliti  juhudi za kupambana na suala la uvuvi haramu katika ziwa Victoria na kusema kuwa siku zao zinahesabika kwa kuwa usaliti ni chanzo cha kurudisha   nyuma mapambano   dhidi ya uvuvi huo. 







TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 Response to "DC SENGEREMA AFUTA BMU ZOTE MAPAMBANO DHIDI YA UVUVI HARAMU."

Post a Comment