DC KAHAMA ASITISHA ZOEZI LA UPIMAJI VIWANJA LILILOKUWA LINALOENDELEA WILAYANI HUMO BAADA YA KUBAINI KUKWEPA KODI YA USHURU WA HUDUMA





NA :SALVATORY KELVIN
Kauli hiyo ameitoa juzi na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Fadhili Nkulu kwenye Baraza la madiwani la halmashauri ya Mji wa Kahama baada ya kuunda kamati ya kufuatilia kero mbalimbali zilizowasilishwa na wananchi mjini humo kuhusia na zoezi la upimaji wa viwanja.
Nkulu amesema kampuni zinazohusika na upimaji wa viwanja mjini Kahama hazijawahi kulipa kodi ya serikali tangu zimeanza kutoa huduma hiyo kwa wananchi huku baadhi makampuni hayo hayana sifa ya kutekeleza zoezi hilo.
Ameongeza kuwa kamati aliyoiunda Imebaini Makampuni hayo kupata zabuni ya kutekeleza zoezi hilo kwa kuwasilisha nyaraka batili kwa kushirikiana na baadhi yawatumishi wa idara ya ardhi ya Halmashauri ya Mji na kuisababishia serikali hasara huku wakijua wazi ni kosa kisheria.
Baadhi ya Kampuni hizo ni pamoja na JMZ Survery limited,Conride survery limited,na nyinginezo ambazo zimepewa zabuni ya kupima viwanja mjini Kahama zote zimezuiliwa kuendelea  na zoezi hilo sanajari na kuwasilisha nyaraka za usajili wao kwa mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji.
Mbali na hilo amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kahama Anderson Msumba kuwachukulia hatua kali wakuu wa idara waandamizi waliotajwa na Ripoti yake ambao ni pamoja mkuu wa idara ya ardhi Joakimu Henjewele na Afisa ardhi mteule Yusuph Luhumba.
Mwisho.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 Response to "DC KAHAMA ASITISHA ZOEZI LA UPIMAJI VIWANJA LILILOKUWA LINALOENDELEA WILAYANI HUMO BAADA YA KUBAINI KUKWEPA KODI YA USHURU WA HUDUMA"

Post a Comment