Na, Paulina Mpiwa, Sengerema Mwanza.
Baadhi ya wananchi wa
mtaa wa Mwabayanda uliopo katika kijiji cha Kizugwangoma Kata ya Misheni Wilayani Sengerema mkoani Mwanza wamelazimika kula mlo mmoja huku wengine wakishindia maembe kutokana na kukosa chakula.
Wamesema licha ya kujitahidi kulima eneo kubwa la mazao mbalimbali
ikiwemo mahindi lakini yamenyauka kwa jua kwa sababu
ya ukame uliokumba
maeneo mengi ya nchi.
Kufuatia hali ya
ukosefu wa chakula wananchi hao wameiomba Serikali kuangalia uwezekano wa kuwasaidia
chakula cha msaada ili kunusuru ukata huo.
Kutokana na hali
hiyo Mulika jamii imemtafuta Mkuu wa wilaya ya Sengerema Bwn,Emmanuel Kipole kuzungumzia suala hili ambapo amesema
serikali ya awamu ya tano
imekwisha toa maelekezo kuwa haitatoa
chakula na badala yake wananchi waendelee kuwa na matumaini huenda mvua zitaendelea kunyeza na kusisitiza
wapande mazao yanayostahimili ukame .
Hata hivyo Agosti 10 ,2016 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt,John
Pombe Magufuli akihutubia mamaia
ya wananchi wa Sengerema
katika uwanja wa mnadani alisema serikali ya awamu ya tano haitakuwa na
huruma ya kutoa chakula kwa watu wanaokichezea.
Awali mamlaka ya hali
ya hewa nchini ilitoa taarifa ya uwepo
wa mvua za wastani katika maeneo mengi ya nchi na kutoa ushauri kwa wananchi
kufuata maelekezo ya wataalamu wa kilimo kwa kulima mazao yanayokomaa muda mfupi
na yanayostahimili ukame ili kuepukana na baa la njaa.
0 Response to "UKAME WAGEUZA MAEMBE KUWA MLO KWA BAADHI YA FAMILIA SENGEREMA."
Post a Comment