WANANCHI WAHOJI TAARIFA ZA MAPATO NA MATUMIZI.


Na, Paulina Mpiwa, Sengerema- Mwanza.

Wakazi wa kitongoji cha KILABELA kata ya MWABALUHI Wilayani SENGEREMA Mkoani MWANZA wamemlalamikia mwenyekiti  wa kitongoji  hicho    kwa kushindwa kuwasomea mapato na matumizi kwa miezi mitatu.

Malalamiko hayo yamekuja kufuatia  wananchi hao kueleza kuwa mwenyekiti huyo amekuwa mstari wa mbele kuchangisha  pesa pasipokujua mchanganua wa fedha hizo wanazochanga kwa shughuli mbalimbali.

Wameeleza kuwa  kiongozi huyo kushindwa kuwasomea mapato na matumizi  ni kudidimiza maendeleo ya eneo  hilo sambamba na kukaribisha mwanya wa upotevu wa fedha  ambazo zingesaidia  katika maendeleo ya kitongoji hicho.

Kufuatia malalamiko hayo mwenyekiti wa kitongoji hicho Bwn. SAMWEL MACHENI NZUNGU amekiri kutowasomea  mapato na matumizi  kwa muda mrefu sasa wananchi wake  huku akiahidi   kutekeleza  jambo hilo hivi karibuni .

Aidha  sakata la mwenyekiti huyo la kutowasomea  taarifa ya mapato na matumizi wakazi wa eneo lake limeanza kuleta taswira mpya baada ya  baadhi ya wakazi  wa eneo hilo kuahidi kutotoa  ushirikiano wa mchango wowote kuanzia hivi sasa mpaka pale atakapofuata utaratibu.


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 Response to "WANANCHI WAHOJI TAARIFA ZA MAPATO NA MATUMIZI."

Post a Comment