Na Salvatory Ntandu :KAHAMA
Jeshi
la Polisi wilayani Kahama linawashikilia watu watano akiwemo mwenyekiti wa
kitongoji cha Iluguti PASCHAL STEPHANO(40) kwaajili ya mahojiano kuhusiana na
tukio la kumtishia kumkata mapanga MINZA SADU (37) kwa kile kinachodaiwa ni
migogoro ya ardhi.
Wengine
ni Pamoja na MASHAKA PETER (25), BULUGU KASU (40) BIS MAKOYE (25) na TABU
MALECHA (40) kwa pamoja wanadaiwa kumpa siku tano MINZA kuhama kijiji hicho na endapo akikaidi wange
muua kwa kumkata mapanaga .
Uamuzi
wa kuawakamata watuhumiwa hao Umetolewa Jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi
na Usalama wa Wilaya ya Kahama, FADHIL NKULU kwenye mkutano wa hadhara na
wakazi wa kijiji cha Nyanhembe kilichopo katika Kata ya Kilago.
NKULU
amesema serikali itaendelea kuchukua hatua kali watu wanaotekeleza mauaji kwa
watu wasiokuwa na hatia kwenye jamii kwa imani za kishirikina jambo ambalo
linapunguza nguvu kazi ya taifa sambamba na kuipa sifa wilaya na mkoa kwa
ujumla.
Kwa
upande wake mkuu wa Polisi Wilaya ya Kahama MUSA MCHENYA ametoa onyo kali kwa
waganga wakienyeji wanaopiga ramli chonganishi kuacha kazi hiyo.
0 Response to "JESHI LA POLISI KAHAMA LANUSURU KUUWAWA KWA MWANAMKE KWA KILE KINACHODAIWA KUWA NI MIGOGORO ARDHI"
Post a Comment