WALIMU WAWILI CHUO CHA UUGUZI SENGEREMA WASABABISHA MGOMO.


Na, Paulina Mpiwa, Sengerema

Wanafunzi wa chuo cha uuguzi SENGEREMA wilayani SENGEREMA  mkoani MWANZA  wameendelea na mgomo wa kutoingia darasani  kushinikiza kuondolewa kwa walimu wawili wanaosababisha migogoro ya mara kwa mara.

Wakizungumza katika kikao cha dharura kilichoitishwa na menejimenti ya chuo kwa lengo la utatuzi wa mgogoro wanachuo hao wamezitaja baadhi ya kero wanazokabiliana nazo kuwa ni pamoja na vitisho kutoka kwa walimu na kula chakula kisichoendana na gharama waliyolipia.

Imeelezwa kuwa Bw,JOHN CHRISTOPHER amekuwa akitoa kauli zisizofaa kwa wanachuo hao, na sista LUCRESIA NJAU anayedaiwa kutokuwa na uwezo wa kufundisha  masomo hasa ya ukunga kitendo kilichopelekea wanafunzi wote kutofaulu katika mtihani wa kanda.
Kwa upande wake mkuu wa chuo hicho Bwana SAMWEL MATHEW amekiri uwepo wa changamoto hizo na kuahidi kuzitatua ili kulinda hadhi ya chuo.

Hata hivyo juhudi ya kuwapata  walimu wanaoshutumiwa hazijazaa matunda baada ya kutokuwa eneo la kikao hicho cha utatuzi wa migogoro.

Kwa upande wake katibu tawala  halmashauri ya wilaya ya SENGEREMA Bwana ALAN MHINA aliyemwakilisha mkuu wa wilaya ya SENGEREMA  katika kikao ameagiza kusimamishwa mara moja Kwa walalamikiwa ili kupisha utatuzi  wa mgogoro huo.

Chuo  cha uuguzi  Sengerema kina milikiwa na kanisa katoliki jimbo la GEITA .


TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 Response to "WALIMU WAWILI CHUO CHA UUGUZI SENGEREMA WASABABISHA MGOMO."

Post a Comment