Na
Paulina Mpiwa, Sengerema.
Jumla ya kaya
46 katika kijiji cha
Bulyaheke Halmashauri
ya Buchosa wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza zimeondolewa katika Mpango
wa kunusuru kaya maskini TASAF awamu ya tatu
kutokana na kutokuwa na
vigezo vinavyotakiwa.
Zoezi hilo
limefanyika chini ya usimamizi
wa Uongozi wa
TASAF ngazi ya wilaya kwa
kushirikiana na viongozi wa eneo husika,
ili kufanya uhakiki
wa kaya ambazo zilitakiwa kuwemo na kutokuwemo, agizo lililotolewa
na serikali ngazi
ya kitaifa.
Baadhi ya
wananchi wamelalamika
kuondolewa katika mpango huo kwani wamedai wanavigezo vya kupata fedha hiyo huku
wengine wakieleza wamesahaulika kuingizwa
ili nao waweze kunufaika kama wengine wanavyoendelea kunufaika.
0 Response to "UHAKIKI WA KAYA MASKINI WALETA SIMANZI."
Post a Comment