TABORA
Na Salvatory Kelvin
Watendaji
wa Serikali mkoani Tabora wametakiwa kuhakikisha kuwa wanakomesha tabia ya
kuwatumikisha watoto wadogo hususan kwenye kilimo cha zao la tumbaku.
Agizo
hilo limetolewa leo na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, AGREY MWANRI wakati akizungumza
kwenye kikao cha wadau wa zao la tumbaku kinachoendelea mkoani humo.
MWANRI
amefafanua kuwa wakuu wa wilaya, wabunge na viongozi mbalimbali wa vyama vya
ushirika wa tumbaku wanapaswa kupiga vita utumikishwaji huo wa watoto
mashambani.
Akizungumza
katika kikao hicho, Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini, EMANUEL MWAKASAKA pamoja
na kuunga mkono kukomesha utumikishwaji wa watoto, amelalamikia msururu wa kodi
kwa wakulima wa tumbaku ambazo hazimnufaishi mkulima.
Zao
la tumbaku licha ya kuliingizia taifa fedha nyingi za kigeni wakulima wa zao
hilo wanakabiliwa na hali duni ya kiuchumi kutokana na wingi wa kodi ambazo
hazimnufaishi mkulima.
0 Response to "SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA KALI WATENDAJI WAZEMBE WANAORUHUSU WATOTO KUTUMIKISHWA KATIKA KILIMO CHA ZAO LA TUMBAKU"
Post a Comment